Posts

MIGUNA MIGUNA MITINI

Hujambo? Miezi michache iliyopita, wakenya na ulimwengu kwa jumla, walipokea habari kutoka kwa aliyekuwa mshauri mkuu wa Waziri Mkuu,Raila Odinga katika serikali ya muungano, bw. Miguna Miguna, kuwa alikuwa akikiandika kitabu kumhusu Raila Odinga. Taarifa hizi zilijiri muda mfupi baada yake kupigwa kalamu. Wengi nikiwa mmoja wao, tulisubiri kwa hamu na ghamu kujua alichotaka kukisema bwana Miguna. Hakusikika kwa muda mrefu. Baadaye aliibuka na kutangaza siku rasmi ya kukizindua kitabu chake. Kabla ya kukizindua rasmi, ujumbe uliokuwa ndani ya kitabu hicho chenye anwani Peeling Back The Mask , ulikuwa tayari katika vyombo vya habari. Ilibainika wazi licha ya ujumbe huo kiduchu kuwa yaliyomo hayakuwa ya Mheshimiwa Raila Odinga tu. Pia waliomo na wasiokuwemo serikalini. Siku ya ndovu kumla mwanawe ilikuwa imefika. Wa kualikwa wakaalikwa na wakususia wakafanya hivyo. Vinani! Bwana Miguna hakutishika. Alizindua kitabu chake mbele ya vyombo vya habari na ulimwengu kwa jumla. Wakat

Ferooz ft Proffesor Jay - Starehe

Image

Ferooz ft Proffesor Jay - Starehe

Image

Matonya - Vailet

Image

Mercy Masika Milele

Image

WEWE PEKEE

Image

KUDORORA KWA KISWAHILI NCHINI

Hujambo? Ninaomba kuichukua nafasi hii kwanza kabisa kuwapongeza ndugu Bitugi Matundura kwa makala yake ya 'Asili ya Kudorora kwa Kiswahili' na Milkah Righa kwa makala yake ya 'Barua kwa Washikadau wa Kiswahili Nchini' ya 06-01-2012. Pili, ni kuwaunga mkono na kujibu baadhi ya maswali mazito yaliyoulizwa na ndugu Milkah Righa. Kudorora kwa Kswahili kote nchini na haswa shuleni, kunachangiwa na mambo mengi. Miongi mwa mambo hayo ni vitabu vya kiada vinavyotumiwa. Ni wazi kuwa Taasisi ya Elimu nchini, imeidhinisha vitabu vingi vinavyotumiwa shuleni. Vitabu vyenyewe vimeandikwa na waandishi mbalimbli ambao wana mitazamo mbalimbali inayokinzana kuhusu kile ambacho wamekiandika. Mifano mizuri ni kuhusu Ngeli za Kiswahili tunazoambiwa kuwa ndio uti wa mgongo wa lugha ya Kiswahili. Waandishi wengi hawana msimamo mmoja wa namna wanavyozianisha na kuzichambua ngeli za Kiswahili.Mathalan, ngeli za A-WA, I-ZI na I-I. Vitabu vingine vinasema kuwa nomino sukari, chumvi,asali, mvua